WUWE

 

 

 

 

  TAASISI YA UELIMISHAJI WANAWAKE YA USAMBARA MAGHARIBI******KUMUELIMISHA MWANAMKE NI KUIELIMISHA JAMII NZIMA!

Aug 6, 2007

UKAUSHAJI WA MBOGA NA MATUNDA

Tangu mwaka 2004, taasisi ya hii imekuwa ikijishughulisha na ukaushaji wa mboga na matunda kwa kutumia kaushio bora la mionzi ya jua. Kaushio hili, limejengwa mfano wa banda kwa kutumia mbao na karatasi ngumu ya nailoni aina ya 'Visquin', ambayo huhifadhi joto linaloingia katika kaushio hilo. Lina matundu maalumu ya kuingizia na kutolea hewa.


Kwa ndani, kaushio hili lina trei maalumu ambazo zimetengenezwa kwa mbao na nyuzi ngumu za nailoni zisizoathiriwa na jua.

Kaushio hili linaweza kukausha mboga, nyama na matunda kwa muda mfupi, iwapo kuna jua la kutosha.

Kaushio la Jua, linavyoonekana kwa nje

Maandalizi ya Matunda (hayo matunda katika beseni ni matufaa)kwa ajili ya ukaushaji. Kwanza yanamenywa, yanaoshwa na kisha hukatwa katika vipande vidogo vidogo ili iwe rahisi kukauka





Matunda yaliandaliwa yakiwekwa katika trei

Matunda yaliyokauka, huondolewa katika kaushio na kuhifadhiwa mahali pakavu kabla ya kufungashwa.

JINA LETU: WUWE
MAHALI TULIPO: LUSHOTO, TANGA, Tanzania
KUHUSU WUWE:
ZAIDI

YALIYOMO

MASKANI
WANACHAMA WETU
WASILIANA NASI

WASHIRIKA WETU

WANACHAMA WETU
TaTEDO
HALMASHAURI YA WILAYA YA LUSHOTO
CAMARTEC

WORLD DAY OF PRAYER
GDS

WUWE

Karibu katika tovuti hii ya WUWE. Hapa tutakuwa tunaweka mada mbali mbali ambazo zinahusiana na kazi zetu, ambazo lengo lake ni kuwasaidia wanawake kwa namna mbalimbali, hasa katika masuala ya elimu na ujasiriamali. Tunaamini kuwa kumwelimisha mwanamke ni kuielimisha jamii nzima, hivyo tukisaidiana kutoa elimu tunaamini tutafanikiwa.

HIFADHI

WUWE





 

MSANIFU: MWALYOYO


©WEST USAMBARA WOMEN EDUCATION (WUWE) 2007. All rights reserved.