UKAUSHAJI WA MBOGA NA MATUNDA
Tangu mwaka 2004, taasisi ya hii imekuwa ikijishughulisha na ukaushaji wa mboga na matunda kwa kutumia kaushio bora la mionzi ya jua. Kaushio hili, limejengwa mfano wa banda kwa kutumia mbao na karatasi ngumu ya nailoni aina ya 'Visquin', ambayo huhifadhi joto linaloingia katika kaushio hilo. Lina matundu maalumu ya kuingizia na kutolea hewa.
Kwa ndani, kaushio hili lina trei maalumu ambazo zimetengenezwa kwa mbao na nyuzi ngumu za nailoni zisizoathiriwa na jua.
Kaushio hili linaweza kukausha mboga, nyama na matunda kwa muda mfupi, iwapo kuna jua la kutosha.
Kaushio la Jua, linavyoonekana kwa nje
Matunda yaliyokauka, huondolewa katika kaushio na kuhifadhiwa mahali pakavu kabla ya kufungashwa.
0 MAONI:
TUMA MAONI
<< REJEA UKURASA MKUU