JIKO LA UKOMBOZI
Jiko hili ni maarufu sana maeneo mengi ya mikoa ya Tanga, Kilimanjaro, Mbeya, Arusha, Pwani, Morogoro na Kagera. Ni jiko la kisasa la kuni, linalotengenezwa kwa kutumia udongo wa kichuguu, samadi mbichi, majivu, maji na majani yanayoteleza. Mchanganyiko huu hufanya jiko hili kutunza joto na hivyo kufupisha muda wa kupika vyakula. Limetengenezwa maalum kuzuia upotevu wa joto na halitoi moshi mwingi kama yalivyo majiko mengine ya asili.
Linatengenezwa kulingana na mahitaji ya mteja. Taasisi ya WUWE imekuwa ikitoa mafunzo kwa mafundi mbali mbali namna ya kutengeneza jiko hili katika mikoa tajwa hapo juu. Mafunzo haya yameonyesha mafanikio, kwani upokeaji wake umekuwa wa kuridhisha.
Picha: Jiko la Ukombozi kabla halijaanza kutumika.
0 MAONI:
TUMA MAONI
<< REJEA UKURASA MKUU