WUWE

 

 

 

 

  TAASISI YA UELIMISHAJI WANAWAKE YA USAMBARA MAGHARIBI******KUMUELIMISHA MWANAMKE NI KUIELIMISHA JAMII NZIMA!

Oct 29, 2007

JIKO LA UKOMBOZI

Jiko hili ni maarufu sana maeneo mengi ya mikoa ya Tanga, Kilimanjaro, Mbeya, Arusha, Pwani, Morogoro na Kagera. Ni jiko la kisasa la kuni, linalotengenezwa kwa kutumia udongo wa kichuguu, samadi mbichi, majivu, maji na majani yanayoteleza. Mchanganyiko huu hufanya jiko hili kutunza joto na hivyo kufupisha muda wa kupika vyakula. Limetengenezwa maalum kuzuia upotevu wa joto na halitoi moshi mwingi kama yalivyo majiko mengine ya asili.
Linatengenezwa kulingana na mahitaji ya mteja. Taasisi ya WUWE imekuwa ikitoa mafunzo kwa mafundi mbali mbali namna ya kutengeneza jiko hili katika mikoa tajwa hapo juu. Mafunzo haya yameonyesha mafanikio, kwani upokeaji wake umekuwa wa kuridhisha.

Picha: Jiko la Ukombozi kabla halijaanza kutumika.

JINA LETU: WUWE
MAHALI TULIPO: LUSHOTO, TANGA, Tanzania
KUHUSU WUWE:
ZAIDI

YALIYOMO

MASKANI
WANACHAMA WETU
WASILIANA NASI

WASHIRIKA WETU

WANACHAMA WETU
TaTEDO
HALMASHAURI YA WILAYA YA LUSHOTO
CAMARTEC

WORLD DAY OF PRAYER
GDS

WUWE

Karibu katika tovuti hii ya WUWE. Hapa tutakuwa tunaweka mada mbali mbali ambazo zinahusiana na kazi zetu, ambazo lengo lake ni kuwasaidia wanawake kwa namna mbalimbali, hasa katika masuala ya elimu na ujasiriamali. Tunaamini kuwa kumwelimisha mwanamke ni kuielimisha jamii nzima, hivyo tukisaidiana kutoa elimu tunaamini tutafanikiwa.

HIFADHI

WUWE





 

MSANIFU: MWALYOYO


©WEST USAMBARA WOMEN EDUCATION (WUWE) 2007. All rights reserved.