SIKU YA KUADHIMISHA JIKO LA UKOMBOZI
Mnamo tarehe 12 Juni 2004, Taasisi ya WUWE ilifanya sherehe za maonesho ya teknolojia mbalimbali ambazo wanashughulika nazo. Teknolojia hizo ni pamoja na majiko sanifu ya kuni na mkaa, oveni za kuchomea nyama, oveni a kuokea mikate, umeme wa jua na majiko ya vikapu yasiyotumia nishati ya moto (majiko bubu) na makaushio bora ya mboga na matunda.
Katika siku hii, viongozi mbali mbali wa serikali na vyama vya siasa walialikwa, pamoja na wananchi wengine kutoka Lushoto mjini na vijiji mbali mbali vya wilaya ya Lushoto. Mgeni rasmi alikuwa ni Bw Mtanga, afisa mipango wa wakati huo wa wilaya ya Lushoto. Ilikuwa ni siku ya kukumbukwa sana, kwani maonesho ya teknolojia za nishati yaliongeza hamasa kwa wananchi kutaka kutumia teknolojia ambazo zilikuwa katika maonesho kwa siku hiyo.
Maandamano, kutoka ofisi za WUWE kwenda ukumbi wa CCM Lushoto
Sheikh Abdi Majaja akisoma utaratibu wa ufunguzi wa sherehe.
Akina mama wakiimba kwaya
Washiriki wakifuatilia hotuba
Afisa kutoka TaTEDO akitoa ufafanuzi jinsi oveni ya kuchomea nyama inavyofanya kazi
Wageni wakiangalia teknolojia za umeme wa jua
Wageni waalikwa wakiangalia bidhaa zilizokaushwa kwa kaushio bora
Wageni wakipata maelezo jinsi oveni ya kuokea mikate inavyofanya kazi
Baadhi ya majiko sanifu ya kuni na mkaa yaliyokuwa katika maonesho
Baadhi ya majiko sanifu ya kuni na mkaa yaliyokuwa katika maonesho
0 MAONI:
TUMA MAONI
<< REJEA UKURASA MKUU